18. Ufalme Uliogawanyika

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 1

Baada ya miaka mingi Daudi alifariki, na mwanae aitwaye Solomoni akatawala Israeli badala yake. Mungu alimuuliza Solomoni kitu muhumu amabcho angetaka apewe. Mungu alimpa Solomoni hekima nyingi kuliko watu wote kama alivyoomba. Naye alijifunza mambo mengi na kutawala kwa haki. Pia Mungu alimpa Solomoni utajiri mwingi.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 2

Katika mji wa Jerusalemu, Solomoni alijenga Hekalu ambayo Baba yake Daudi alikusudia kuujenga na hivyo kuandaa vifaa vya ujenzi. Watu walianza kumuabudu na kumtolea Mungu sadaka ndani ya Hekalu badala ya kwenye hema ya kukutania. Mungu alishuka na kukaa ndani ya hekalu na kuishi pamoja na watu wake.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 3

Lakini Solomoni aliwapenda wanawake wa mataifa mengine .Hakumtii Mungu kwa kuwaoa wanawake wengi. Aliwaoa karibu wake 1000. Hao wanawake waliolewa na Solomoni kutoka mataifa mengine walileta na kuaendelea kuabudu miungu yao . Hata Solomoni alipokuwa mzee, naye akaabudu hizo miungu.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 4

Mungu alimkasirikia Solomoni, na kukusudia kumuadhibu kwasababu ya kukosa uaminifu. Hivyo Mungu akaahidi kugawa Taifa la Israeli kuwa falme mbili baada ya kifo chake.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 5

Baada ya Solomoni kufa, Rehoboamu mwanaye , akawa Mfalme. Rehoboamu alikuwa mfalme mpumbavu , watu wote wa Israeli walimridhia yeye kuwa mfalme wao. Watu walimjia na kumlalamikia kuwa Baba yake Solomoni aliwatesa kwa kazi ngumu na kuwatoza gharama kubwa ya kodi.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 6

Mfalme Rehoboamu aliwajibu kwa upumbavu kuwa , msidhani ya kuwa baba yangu aliwapa ninyi kazi nguu , kwani mimi nitawafanya ninyi mfanye kazi ngumu zaidi kuliko alizowapa Baba yangu na kuwapatia ninyi adhabu zaidi kuliko yale ya Baba yangu.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 7

Makabila kumi ya Taifa la Israeli yalimuasi mfalme Rehoboamu , na makabila mawili yaliendelea kuwa waaminifu kwake. Hayo makabila mawili yaliunda ufalme wa Yuda.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 8

Makabila yale kumi ya Israeli yaliyo muasi Rehoboamu, waliungana na kumchagua mtu aitwaye Jeroboamu kuwa mfalme wao. Wao walikaa kazikazini mwa nchi ya Israeli. Makabila hayo kumi yaliunda ufalme wa Israeli.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 9

Jeroboamu alimuasi Mungu a kuwafanya watu kutenda dhambi. Alitengeneza sanamu mbili na kuwafanya watu kuiabudu badala ya kumuabudu Mungu wa kweli anayeabuduiwa katika Hekalu lililoko Yuda.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 10

Ufalme wa Yuda na Israeli wakawa maadui, na mara nyingi hupigana wao kwa wao

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 11

Katika Ufalme mpya wa Israeli wafalme wote walikuwa waovu, na wafalme wengi waliuwawa na waisraeli waliotaka kuwa wafalme badala yao

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 12

Wafalme wote , na watu wengi waliopo katika ufalme wa Israeli waliabudu sanamu. Baadhi ya vitu walivyoabudu ni pamoja na uzinzi na kutoa kafara ya watoto wao.

18. Ufalme Uliogawanyika — picha 13

Wafalme wa Yuda ni wazaliwa wa Daudi, baadhi ya wafalme hao waliongoza kwa haki na kumuabudu Mungu, hata hivyo wengi wa wafalme wa Yuda walikuwa waovu na walarushwa, baadhi yao hutoa watoto wao kama kafara kwa miungu. Pia watu wengi wa ufalme wa Yuda walimuasi Mungu na kuabudu miungu mingine.

Simulizi ya Biblia kutoka: 1Wafalme 1-6; 11-12

Soma katika kisomaji

Bila malipo kutumia, kubadilisha na kushiriki chini ya leseni huria (CC BY-SA 4.0).